Mama yake Vozinha awasili Praia kabla ya safari ya Marekani
Mama yake kipa mkongwe wa Cape Verde Vozinha amewasili
katika mji mkuu wa nchi hiyo Praia kujiandaa kwa safari yake ya kuelekea
Marekani.
Ana Cândida Évora aliondoka katika mji wake wa São
Vicente Jumatano usiku, akiandamana na mbunge anayewakilisha wilaya yake.
BBC inafahamu kuwa Bi Évora anaweza kuwasili Marekani
kati ya Ijumaa na Jumamosi, kabla ya mchuano wa Jumapili kati ya Cape Verde na
Uruguay huko Miami.
"Nina furaha," aliiambia BBC, akionyesha
matumaini kwamba kila kitu kitaenda sawa.
"Ninabeba ujasiri wa kipekee kwa raia wa Cape Verde walioko
huko. Tutapambana na kung'ara kwenye uwanja huo," aliongeza.
Kwenye uwanja wa ndege wa São Vicente, aliwakumbatia wanafamilia
na wapendwa wake kabla ya kuelekea Praia.
Utafiti waonesha mafanikio makubwa ya chanjo ya saratani ya shingo ya kizazi
Chanzo cha picha, Unicef
Takriban maisha ya watu 200 yameokolewa nchini Uingereza
kufikia sasa kutokana na chanjo inayokinga saratani ya shingo ya kizazi, hii
ikiwa ni kulingana na uchambuzi uliochapishwa katika jarida la la Lancet.
Utafiti huo wa kwanza wa aina yake umeonyesha kwamba
vifo vimepungua sana tangu wasichana wenye umri wa kwenda shule walipopewa
chanjo ya human papillomavirus (HPV) mwaka 2008.
Ripoti ya utafiti huo inaonesha kuwa kati ya 2020 na 2024,
hakuna vifo vya saratani ya shingo ya kizazi vilirekodiwa kwa wanawake wenye
umri wa miaka 20 hadi 24 - mara ya kwanza kutokea kwa kipindi cha miaka mitano.
Bila chanjo,
takribani vifo ishirini na vitatu vingetarajiwa.
Prof Peter
Sasieni, mtafiti mkuu katika Chuo Kikuu cha Queen Mary cha London amesema:
"Inashangaza
kufikiria kwamba chanjo inaweza kukaribia kumaliza aina fulani ya
saratani,"
Utafiti huo pia
uligundua kuwa watoto hao waliochanjwa wakiwa na umri wa miaka 12 au 13 sasa
hawakabiliwi kabisa na hatari ya kufariki dunia kutokana na ugonjwa huo kabla
ya umri wa miaka 30.
Kabla ya kampeni
ya chanjo ya HPV, takribani vifo 20 kila mwaka vilikuwa vikirekodiwa katika
kundi hilo la umri.
Kwa ujumla,
saratani ya shingo ya kizazi bado ni saratani ya 14 kati ya wanawake nchini
Uingereza, na watu 3,300 hugunduliwa kila mwaka.
Inafikiriwa kuwa
HPV, virusi ambavyo huenezwa kwa mgusano wa karibu wa ngozi kwa ngozi,
husababisha asilimia 99 ya maaambukizi yote ya saratani hiyo.
Maambukizi mengi
ya HPV hupita bila matatizo yoyote, lakini mengine husababisha mabadiliko
yasiyo ya kawaida ya seli na yanaweza kusababisha saratani miaka mingi baadaye.
Ruto awaalika Arsenal Kenya baada ya sherehe za kukata na shoka
Chanzo cha picha, Getty Images
Rais William
Ruto amewaalika mabingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza Arsenal kutembelea Kenya
kufuatia sherehe zilizojumuisha shangwe, nderemo na vifijo kutoka kwa mashabiki
wao baada ya klabu hiyo kumaliza kiu ya muda mrefu kwa kupata ushindi wa taji
la ligi.
Rais alisema
alishangazwa na ukubwa wa sherehe zilizoshuhudiwa jijini Nairobi baada ya
Arsenal kutwaa ubingwa.
Akizungumza
na Reuters wakati wa Mkutano wa G7 nchini Ufaransa, Rais alibainisha kuwa
msisimko miongoni mwa mashabiki wa Kenya ulimfanya afuatilie uwezekano wa
kuileta klabu hiyo ya Kaskazini mwa London nchini humo mwaka ujao.
abu hiyo.
Chanzo cha picha, AFP via Getty Images
"Arsenal hatimaye ilipata ubingwa, na kuwa sherehe kubwa. Nilishangaa sana kilichotokea jijini Nairobi," Ruto alisema.
"Ilikuwa sherehe kubwa, najaribu kufuatilia kama Arsenali wanaweza kuja nchini mwaka ujao. Nimetuma mwaliko kwa sababu nafikiria itakuwa wakati mzuri kwa Arsenal kuja Kenya. Wana mashabiki wa kipekee."
Kenya ni mojawapo ya nchini zenye mashabiki wengi wa Arsenal barani Afrika na mashabiki hukusanyika mara kwa mara katika miji mikubwa mbalimbali kutazama mechi za kl
Maelezo ya picha, Shabiki wa Arsenal
Ushindi wa taji la Gunners ulisababisha sherehe kote nchini Kenya, huku mashabiki wakijitokeza mitaani, katika mitandao ya kijamii na sehemu za burudani kuadhimisha ushindi wa kihistoria wa klabu hiyo.
Urusi na Ukraine zashambuliana huku Zelensky akizungumza na Trump, Ulaya
Chanzo cha picha, Reuters
Urusi imeshambulia Kyiv kwa makombora na ndege zisizo na
rubani za Ukraine katika kiwanda cha kusafishia mafuta cha Moscow huku nchi
zote mbili zikishambuliana saa chache baada ya Rais Volodymyr Zelensky
kuzungumza na Rais wa Marekani Donald Trump na viongozi wa Ulaya.
Kwa mujibu wa Reuters alisikia milipuko huko Kyiv na mamlaka
katika mji wa Sumy kaskazini mashariki mwa Ukraine zilisema mtu mmoja aliuawa
katika shambulio la ndege isiyo na rubani.
Tahadhari za mashambulizi ya anga zilitolewa kwa eneo kubwa
la Ukraine.
"Adui anashambulia mji mkuu kwa makombora ya balestiki.
Kaeni katika maeneo salama hadi tahadhari ya uvamizi wa anga itakapoondolewa!"
Tymur Tkachenko, mkuu wa utawala wa kijeshi wa Kyiv, alisema katika chapisho la
Telegram mapema Alhamisi.
Shambulio dhidi ya Kyiv ni la pili wiki hii na limetokea huku
Zelensky akijaribu kuongeza shinikizo kwa Urusi ili kujadili kukomesha vita
vyake vya miaka minne.
Katika mji mkuu wa Urusi, ndege zisizo na rubani zilishambulia
kiwanda cha kusafishia mafuta cha Moscow, Meya Sergei Sobyanin alisema kwenye
Telegram, akiashiria shambulio la pili kwenye kituo hicho ndani ya wiki moja.
Kombe la Dunia 2026: Vozinha kujumuika na mama yake
Chanzo cha picha, Getty Images
Mama wa kipa wa Cape Verde, Vozinha, amepewa viza ya
kusafiri kwenda Marekani ili kumtazama mwanawe katika michuano ya Kombe la
Dunia.
Tangazo hilo lilitolewa na Kiongozi wa chama cha Democrat
katika Baraza la Wawakilishi, Hakeem Jeffries, ambaye alisema amezungumzia
suala hilo binafsi na Waziri wa Mambo ya Nje, Marco Rubio.
Vozinha alijipatia umaarufu mapema katika michuano hiyo
baada ya kuokoa timu yake isifungwe mara saba katika mchezo ambao Cape Verde na
kutoka sare tasa ya kushtusha dhidi ya Uhispania.
Baada ya mchezo huo, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 40
alisema mama yake alishindwa kuhudhuria michuano hiyo kwa sababu ya gharama kubwa ya kupata viza ya
Marekani.
Bw. Jeffries amesema ada zimefutwa na mipango ya safari sasa
inaandaliwa ili mama huyo aweze kumtazama mwanawe akicheza dhidi ya Uruguay
mjini Miami siku ya Jumapili.
Mama yake pia aliithibitishia BBC akiwa nyumbani kwake huko
Sao Vicente kwamba mipango ilikuwa imefanywa ili asafiri hadi Miami.
"Nina furaha sana," alisema Ana Candida Evora.
"Hili linatokea haraka sana, lakini nina furaha mno.
Nitamuona mwanangu akicheza Kombe la Dunia, Mungu akipenda."
"Ninaenda huko kumsaidia, kumpa nguvu na ujasiri.
Nitamkumbatia baada ya mchezo."
Kombe la Dunia 2026: Ghana yafunga bao la ushindi dakika ya 95
Chanzo cha picha, Getty Images
Fainali za Kombe
la Dunia huko Marekani, Mexico na Canada zinazidi kupamba moto.
Umekuwa usiku
wenye ahueni kubwa kwa bara la Afrika, ambalo wawakilishi wake wawili walikuwa
dimbani: Ghana imefanikiwa kupata alama 3 baada ya kuichapa Panama 1-0.
Goli hilo la pekee
katika mchezo uliopigwa usiku wa manane limepachkwa naCaleb
Yirenky katikadakika ya tisini ya mchezo huko Toronto Canada.
Ghana ni timu ya
pili kupata ushindi miongoni mwa wawakilishi 10 wa Afrika, nyingine ni Ivory
Coast.
Timu nyingine 4
zimepata sare huku 4 zikichezea vichapo.
Awali, Jamhuri ya
Kidemokras ya Congo ilionesha mbinu za hali ya juu za ulinzi na nidhamu kubwa
ya mchezo na kufanikiwa kupata alama 1 mbele ya moja ya vigogo vya soka duniani
Ureno, kwa sare ya goli 1-1.
Hiyo ni alama na
goli la kwanza katika fainali za Kombe la Dunia kwa DRC iliyorejea baada ya
miaka 52, kwani waliposhiriki kwa mara ya kwanza mwaka 1974 huko Ujerumani,
walipoteza michezo yote mitatu ya hatua ya makundi bila kufunga bao.
Kwa upande
mwingine, mabingwa wa dunia wa mwaka 1966, England wamejipatia ushindi wa 4-2
dhidi ya washindi wa pili wa fainali za 2018, Croatia.
Magoli ya Harry
Kane aliyepachika mawili na Jude Bellingham na Marcus Rashford yalitosha kuipa
ushindi England huku mawili ya Croatia yakitiwa kimiani na Martin Baturina na
Petar Mussa.
Kombe la Dunia 2026: Díaz aisaidia Colombia kupata ushindi dhidi ya Uzbekistan
Chanzo cha picha, Getty Images
Pambano
lililomalizika saa moja asubuhi hii kati ya Uzbekistan wanaoshiriki kwa mara ya
kwanza na Colombia wanaorejea baada ya kushindwa kufuzu huko Qatar 2022.
Luis Díaz alifunga bao na kutoa pasi ya bao katika mechi
yake ya kwanza kwenye jukwaa kubwa zaidi la soka, na kuiwezesha Colombia
kushinda 3-1 dhidi ya Uzbekistan katika mchezo wake wa ufunguzi wa Kombe
la Dunia.
Daniel Muñoz, ambaye pia alicheza katika Kombe la Dunia kwa
mara ya kwanza, alifungua ukurasa wa mabao dakika ya 40 baada ya pasi kutoka
kwa Díaz, ambaye alifunga bao la kusawazisha dakika ya 65.
Fayzullaev Abbosbek amefunga bao dakika ya 60 kwa Uzbekistan
katika mechi yake ya kwanza ya Kombe la Dunia.
Jaminton Campaz aliongeza bao katika kipindi cha pili kwa
Wakolombia, ambao wako katika nafasi ya 13 duniani na walikuwa na nafasi kubwa
ya kushinda kuliko Uzbekistan iliyo katika nafasi ya 50.
Colombia ilipanda kileleni mwa Kundi K, mbele ya Ureno na
Congo, ambazo zilitoka sare ya kushangaza ya 1-1 mapema Jumatano.
Trump na rais wa Iran watia saini mkataba wa awali unaolenga kumaliza vita
Chanzo cha picha, Getty Images/SOPA Images
Viongozi wa Marekani na Iran wamesaini makubaliano ya awali
ya amani yanayolenga kukomesha vita hivyo, na kuanza kutekelezwa mara moja.
Mkataba huo unajumuisha kufungua tena Mlango-Bahari wa
Hormuz, mpango wa dola bilioni 300 (£224bn) kwa ajili ya "ujenzi
mpya" wa Iran, na Marekani kukomesha "aina zote za vikwazo"
dhidi ya Iran.
Lakini suala la mpango wa nyuklia wa Iran, sababu kuu
iliyotajwa na Marekani kwa mzozo huo, bado halijajadiliwa kwa muda wa siku 60 za
kusitisha mapigano ulioongezwa.
Chanzo cha picha, Reuters
Rais wa Marekani Donald Trump, ambaye alisaini makubaliano hayo nchini Ufaransa wakati wa mkutano wa kilele wa G7, alitetea pendekezo hilo, akisema litaepusha "janga la kiuchumi". Hata hivyo, alionya kwamba Marekani "itaishambulia" Iran ikiwa hakuna makubaliano ya mwisho yatakayofikiwa.
Rais wa Iran Masoud Pezeshkian pia alisaini hati hiyo Jumatano, Tehran ilithibitisha.
Spika wa bunge la Iran na mjumbe mkuu wa mazungumzo Mohammad Bagher Ghalibaf aliviambia vyombo vya habari vya serikali kwamba imani yake kwa Marekani bado ipo, na Iran "iko katika hali ya tahadhari".
"Ikiwa adui haelewi lugha ya mantiki, tutaingia tena na lugha ya nguvu," aliambia chombo cha habaro cha serikali cha Fars.
Marekani na Israel zilianzisha vita dhidi ya Iran mnamo tarehe 28 Februari, na kumuua Kiongozi Mkuu Ayatollah Ali Khamenei na maafisa wakuu wa kijeshi siku ya kwanza.
Trump aliwaambia waandishi wa habari nchini Ufaransa katika eneo la mapumziko la Evian-les-Bains kando ya ziwa, ambapo mkutano wa kilele wa G7 uliandaliwa, kwamba mpango huo utaepusha " dhiki kwa dunia nzima".
"Sikutaka kuona janga la kiuchumi," Trump aliwaambia waandishi wa habari. "Kama ungeendelea hivi, hilo lingetokea."