Moja kwa moja, Trump na rais wa Iran watia saini mkataba wa awali unaolenga kumaliza vita

Mpango wa nyuklia wa Iran, sababu kuu iliyotajwa na Marekani kwa mzozo huo, bado unajadiliwa.

Muhtasari

Skip Video and continue reading
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • xx
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Asha Juma

  1. Utafiti waonesha mafanikio makubwa ya chanjo ya saratani ya shingo ya kizazi

    .

    Chanzo cha picha, Unicef

    Takriban maisha ya watu 200 yameokolewa nchini Uingereza kufikia sasa kutokana na chanjo inayokinga saratani ya shingo ya kizazi, hii ikiwa ni kulingana na uchambuzi uliochapishwa katika jarida la la Lancet.

    Utafiti huo wa kwanza wa aina yake umeonyesha kwamba vifo vimepungua sana tangu wasichana wenye umri wa kwenda shule walipopewa chanjo ya human papillomavirus (HPV) mwaka 2008.

    Ripoti ya utafiti huo inaonesha kuwa kati ya 2020 na 2024, hakuna vifo vya saratani ya shingo ya kizazi vilirekodiwa kwa wanawake wenye umri wa miaka 20 hadi 24 - mara ya kwanza kutokea kwa kipindi cha miaka mitano.

    Bila chanjo, takribani vifo ishirini na vitatu vingetarajiwa.

    Prof Peter Sasieni, mtafiti mkuu katika Chuo Kikuu cha Queen Mary cha London amesema:

    "Inashangaza kufikiria kwamba chanjo inaweza kukaribia kumaliza aina fulani ya saratani,"

    Utafiti huo pia uligundua kuwa watoto hao waliochanjwa wakiwa na umri wa miaka 12 au 13 sasa hawakabiliwi kabisa na hatari ya kufariki dunia kutokana na ugonjwa huo kabla ya umri wa miaka 30.

    Kabla ya kampeni ya chanjo ya HPV, takribani vifo 20 kila mwaka vilikuwa vikirekodiwa katika kundi hilo la umri.

    Kwa ujumla, saratani ya shingo ya kizazi bado ni saratani ya 14 kati ya wanawake nchini Uingereza, na watu 3,300 hugunduliwa kila mwaka.

    Inafikiriwa kuwa HPV, virusi ambavyo huenezwa kwa mgusano wa karibu wa ngozi kwa ngozi, husababisha asilimia 99 ya maaambukizi yote ya saratani hiyo.

    Maambukizi mengi ya HPV hupita bila matatizo yoyote, lakini mengine husababisha mabadiliko yasiyo ya kawaida ya seli na yanaweza kusababisha saratani miaka mingi baadaye.

    Soma zaidi:

  2. Urusi na Ukraine zashambuliana huku Zelensky akizungumza na Trump, Ulaya

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Urusi imeshambulia Kyiv kwa makombora na ndege zisizo na rubani za Ukraine katika kiwanda cha kusafishia mafuta cha Moscow huku nchi zote mbili zikishambuliana saa chache baada ya Rais Volodymyr Zelensky kuzungumza na Rais wa Marekani Donald Trump na viongozi wa Ulaya.

    Kwa mujibu wa Reuters alisikia milipuko huko Kyiv na mamlaka katika mji wa Sumy kaskazini mashariki mwa Ukraine zilisema mtu mmoja aliuawa katika shambulio la ndege isiyo na rubani.

    Tahadhari za mashambulizi ya anga zilitolewa kwa eneo kubwa la Ukraine.

    "Adui anashambulia mji mkuu kwa makombora ya balestiki. Kaeni katika maeneo salama hadi tahadhari ya uvamizi wa anga itakapoondolewa!" Tymur Tkachenko, mkuu wa utawala wa kijeshi wa Kyiv, alisema katika chapisho la Telegram mapema Alhamisi.

    Shambulio dhidi ya Kyiv ni la pili wiki hii na limetokea huku Zelensky akijaribu kuongeza shinikizo kwa Urusi ili kujadili kukomesha vita vyake vya miaka minne.

    Katika mji mkuu wa Urusi, ndege zisizo na rubani zilishambulia kiwanda cha kusafishia mafuta cha Moscow, Meya Sergei Sobyanin alisema kwenye Telegram, akiashiria shambulio la pili kwenye kituo hicho ndani ya wiki moja.

    Soma zaidi:

  3. Kombe la Dunia 2026: Ghana yafunga bao la ushindi dakika ya 95

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Fainali za Kombe la Dunia huko Marekani, Mexico na Canada zinazidi kupamba moto.

    Umekuwa usiku wenye ahueni kubwa kwa bara la Afrika, ambalo wawakilishi wake wawili walikuwa dimbani: Ghana imefanikiwa kupata alama 3 baada ya kuichapa Panama 1-0.

    Goli hilo la pekee katika mchezo uliopigwa usiku wa manane limepachkwa naCaleb Yirenky katikadakika ya tisini ya mchezo huko Toronto Canada.

    Ghana ni timu ya pili kupata ushindi miongoni mwa wawakilishi 10 wa Afrika, nyingine ni Ivory Coast.

    Timu nyingine 4 zimepata sare huku 4 zikichezea vichapo.

    Awali, Jamhuri ya Kidemokras ya Congo ilionesha mbinu za hali ya juu za ulinzi na nidhamu kubwa ya mchezo na kufanikiwa kupata alama 1 mbele ya moja ya vigogo vya soka duniani Ureno, kwa sare ya goli 1-1.

    Hiyo ni alama na goli la kwanza katika fainali za Kombe la Dunia kwa DRC iliyorejea baada ya miaka 52, kwani waliposhiriki kwa mara ya kwanza mwaka 1974 huko Ujerumani, walipoteza michezo yote mitatu ya hatua ya makundi bila kufunga bao.

    Kwa upande mwingine, mabingwa wa dunia wa mwaka 1966, England wamejipatia ushindi wa 4-2 dhidi ya washindi wa pili wa fainali za 2018, Croatia.

    Magoli ya Harry Kane aliyepachika mawili na Jude Bellingham na Marcus Rashford yalitosha kuipa ushindi England huku mawili ya Croatia yakitiwa kimiani na Martin Baturina na Petar Mussa.

    Soma zaidi:

  4. Kombe la Dunia 2026: Díaz aisaidia Colombia kupata ushindi dhidi ya Uzbekistan

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Pambano lililomalizika saa moja asubuhi hii kati ya Uzbekistan wanaoshiriki kwa mara ya kwanza na Colombia wanaorejea baada ya kushindwa kufuzu huko Qatar 2022.

    Luis Díaz alifunga bao na kutoa pasi ya bao katika mechi yake ya kwanza kwenye jukwaa kubwa zaidi la soka, na kuiwezesha Colombia kushinda 3-1 dhidi ya Uzbekistan katika mchezo wake wa ufunguzi wa Kombe la Dunia.

    Daniel Muñoz, ambaye pia alicheza katika Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza, alifungua ukurasa wa mabao dakika ya 40 baada ya pasi kutoka kwa Díaz, ambaye alifunga bao la kusawazisha dakika ya 65.

    Fayzullaev Abbosbek amefunga bao dakika ya 60 kwa Uzbekistan katika mechi yake ya kwanza ya Kombe la Dunia.

    Jaminton Campaz aliongeza bao katika kipindi cha pili kwa Wakolombia, ambao wako katika nafasi ya 13 duniani na walikuwa na nafasi kubwa ya kushinda kuliko Uzbekistan iliyo katika nafasi ya 50.

    Colombia ilipanda kileleni mwa Kundi K, mbele ya Ureno na Congo, ambazo zilitoka sare ya kushangaza ya 1-1 mapema Jumatano.

    Soma zaidi:

  5. Trump na rais wa Iran watia saini mkataba wa awali unaolenga kumaliza vita

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Viongozi wa Marekani na Iran wamesaini makubaliano ya awali ya amani yanayolenga kukomesha vita hivyo, na kuanza kutekelezwa mara moja.

    Mkataba huo unajumuisha kufungua tena Mlango-Bahari wa Hormuz, mpango wa dola bilioni 300 (£224bn) kwa ajili ya "ujenzi mpya" wa Iran, na Marekani kukomesha "aina zote za vikwazo" dhidi ya Iran.

    Lakini suala la mpango wa nyuklia wa Iran, sababu kuu iliyotajwa na Marekani kwa mzozo huo, bado halijajadiliwa kwa muda wa siku 60 za kusitisha mapigano ulioongezwa.

    Rais wa Marekani Donald Trump, ambaye alisaini makubaliano hayo nchini Ufaransa wakati wa mkutano wa kilele wa G7, alitetea pendekezo hilo, akisema litaepusha "janga la kiuchumi". Hata hivyo, alionya kwamba Marekani "itaishambulia" Iran ikiwa hakuna makubaliano ya mwisho yatakayofikiwa.

    Rais wa Iran Masoud Pezeshkian pia alisaini hati hiyo Jumatano, Tehran ilithibitisha.

    Spika wa bunge la Iran na mjumbe mkuu wa mazungumzo Mohammad Bagher Ghalibaf aliviambia vyombo vya habari vya serikali kwamba imani yake kwa Marekani bado ipo, na Iran "iko katika hali ya tahadhari".

    "Ikiwa adui haelewi lugha ya mantiki, tutaingia tena na lugha ya nguvu," aliambia chombo cha habaro cha serikali cha Fars.

    Marekani na Israel zilianzisha vita dhidi ya Iran mnamo tarehe 28 Februari, na kumuua Kiongozi Mkuu Ayatollah Ali Khamenei na maafisa wakuu wa kijeshi siku ya kwanza.

    Trump aliwaambia waandishi wa habari nchini Ufaransa katika eneo la mapumziko la Evian-les-Bains kando ya ziwa, ambapo mkutano wa kilele wa G7 uliandaliwa, kwamba mpango huo utaepusha " dhiki kwa dunia nzima".

    "Sikutaka kuona janga la kiuchumi," Trump aliwaambia waandishi wa habari. "Kama ungeendelea hivi, hilo lingetokea."

    Soma zaidi:

  6. Hujambo na karibu katika matangazo yetu mubashara. Tarehe ni 18/06/2026.