Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani: Tuko tayari kwa mazungumzo, lakini Iran haina nia ya dhati

Chanzo cha picha, Getty Images
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio, amesema kuwa iwapo Iran itadhibiti Mlango-Bahari wa Hormuz, hali hiyo itasababisha "mwelekeo hatari" kwa usalama na biashara ya kimataifa.
Akizungumza katika mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa nchi za Kusini Mashariki mwa Asia, Rubio alisema Marekani bado iko tayari kufanya mazungumzo ya kumaliza mgogoro na Iran, lakini alidai kuwa Tehran haijaonesha nia ya dhati ya kushiriki mazungumzo hayo.
Kauli zake zinakuja wakati kuongezeka kwa mzozo huo kumeathiri njia mbili muhimu za usafirishaji wa nishati duniani.
Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, afisa mmoja mwandamizi wa Iran alisema Jumatatu kwamba Tehran imepokea pendekezo kutoka kwa wapatanishi la kusitisha mapigano kwa muda wa siku 10.
Jana, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Iran alisafiri kwenda Pakistan kwa mazungumzo na Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Shehbaz Sharif, pamoja na Mkuu wa Jeshi, Jenerali Asim Munir. Viongozi hao wawili wamekuwa miongoni mwa wapatanishi wakuu katika mazungumzo kati ya Iran na Marekani.
Unaweza kusoma;
























