Rais wa Namibia Netumbo Nandi - Ndaitwah amaliza kulipa deni lote la IMF
Rais wa Namibia, Netumbo Nandi‑Ndaitwah, ameiongoza nchi yake kufikia hatua muhimu ya kiuchumi kwa kukamilisha malipo ya deni la Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF).
Namibia imelipa jumla ya dola milioni 23.9, hatua inayolenga kupunguza mzigo wa madeni ya nje na kuimarisha uthabiti wa uchumi wa taifa hilo.
Kukamilika kwa deni hili kunatajwa kuongeza uhuru wa kifedha wa Namibia na kuipa serikali nafasi pana zaidi ya kuelekeza rasilimali zake katika miradi ya maendeleo ya ndani.
Hatua hii imepokelewa kama ushindi mkubwa katika usimamizi wa fedha za umma chini ya uongozi uliopo, ikionyesha uthabiti wa kiuchumi wa nchi hiyo katika ukanda wa Kusini mwa Afrika. Kwa mujibu wa takwimu hadi Machi mwaka huu, malipo hayo yamefikia jumla ya dola milioni 23.8875.
Namibia sasa imejiunga na mataifa mengine ya Afrika, ikiwemo Msumbiji, ambayo yamefanikiwa kufuta madeni yao kwa IMF, ikifuata mwenendo wa kupunguza mikopo ya nje na kuimarisha nidhamu ya kifedha.
Akiwa na umri wa miaka 72 rais wa kwanza mwanamke Namibia alishinda uchaguzi kwa 57% ya kura huku mpinzani wake wa karibu Panduleni Itula akipata 26% ya kura, kulingana na tume ya uchaguzi nchini humo.
Netumbo Nandi-Ndaitwah ameingia madarakani mwezi Disemba 2024.