Trump: Huenda tukashambulia Mlima Kalang hivi karibuni

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images
Siku ya Ijumaa, Donald Trump aliwaambia waandishi wa habari kuwa Marekani inaweza kuushambulia Mlima Kalang nchini Iran hivi karibuni.
Mlima Kalang, uliopo karibu na kituo cha kurutubisha urani cha Natanz, ni eneo lililolindwa sana la kijeshi lenye mifumo miwili ya mahandaki ya kina kirefu.
Katika sehemu nyingine ya maelezo yake, Rais huyo wa Marekani alisema kuwa vita dhidi ya Iran ni "jambo dogo" kwa Marekani.
Awali, Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance alisema siku ya Alhamisi kuwa asingeliita mgogoro na Iran kuwa ni "vita."
Siku ya Ijumaa, Donald Trump alitoa ufafanuzi alipoulizwa na mwandishi wa habari awaeleze wananchi wa Marekani maana ya vita na Iran ikiwa hali hiyo haitaitwa "vita", alisema, "Naam, nawaambia, watu wengi hawaiiti hali hi kuwa vita.
Mimi naiita mgogoro wa kijeshi, kwa sababu kwetu sisi ni jambo dogo kiasi. Sio jambo kubwa. Tulichukua hatua nchini Venezuela na tukafanikiwa. Hatukupoteza maisha ya watu nchini Venezuela.
Tulipoteza watu 18 katika mgogoro na Iran. Tulipoteza watu 100,000 nchini Vietnam."

