Moja kwa moja, Tume ya uchunguzi yasema watu 518 walifariki dunia wakati wa ghasia za uchaguzi Tanzania

Ripoti hii inachukuliwa kama nyenzo muhimu ya kuweka wazi ukweli na kutoa mwelekeo wa taifa baada ya kipindi hicho kigumu.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Martha Saranga, Rashid Abdallah & Ambia Hirsi

  1. 'Chombo kitakachoundwa kitaangazia taarifa za wanaodaiwa kutekwa ambao bado hawajapatikana'

    Rais Samia amesema chombo maalum cha upelelezi kitakachoundwa kwa ajili ya kufanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa na tume kitajielekeza kuangazia masuala kadhaa ikiwemo masuala ya wanaodaiwa kutekwa ambao taarifa zao bado hazijapatikana.

    Aidha chombo hicho kitaangalia na kubaini waliohusika kuratibu kupanga na kufadhili matukio ya ghasia za Oktoba29.

    'Vilevile watajielekeza kubaini matukio ya vurugu na uhalifu,kwa bahati nzuri picha zipo'alieleza

    Pia chombo hicho kitaangazia miili ambayo haijapatikana na walioathirika nje ya maeneo ya vurugu.

  2. 'Hii ni ripoti ya rais' - rais Samia

    Samia

    Chanzo cha picha, IKULU

    Rais Samia amesema ripoti hii ni ya rais aliyeunda tume husika.

    Akizungumza baada ya kusikiliza uwasilishwaji wa ripoti hiyo alisema 'Tumesikia masuala yaliyobainishwa na tume'

    Hii ni ripoti ya rais kwahiyo wasitokee watu wengine wakadai ownership ya ripoti hii'

    Aidha ameahidi kuanza kufanyia kazi mara moja mapendekezo yaliyotolewa na tume hiyo.'Katika muda mfupi ujao serikali itaunda tume ya maridhiano ikijumuisha wadau wote muhimu ili kuziba mianya na kurejesha umoja wa kitaifa.

  3. 'Bado tunajifunza na kukua katika mfumo wa demokrasia'- Samia Rais

    Rais Samia amesema bado Tanzania inajifunza na kukua katika mfumo wa vyama vingi.

    'Demokrasia haina budi kujengwa kwa kuzingatia mazingira ya nchi mila tamaduni za nchi husika nakuongeza kuwa kwa misingi hiyo ‘tuachwe tujenge demokrasia yetu kwa desturi yetu mila na tamaduni zetu'

    Ndugu zangu mliponikabidhi dhamana ya kuongoza nchi nilibaini kuwepo kwa changamoto katika mifumo ya demokrasia ya vyama vingi nchini.

    Rais Samia amerejelea malalamiko mengi kutoka kwa wadau wa siasa kuhusu kunyimwa uhuru wa kisiasa, uhuru wa kujieleza na changamoto katika mifumo ya uchaguzi akieleza kwamba kupitia falsafa ya 4R hatua kadhaa zilichukuliwa ikiwemo kuundwa kwa kikosi kazi cha kushughulikia changamoto hizo.

  4. Tume ya Uchunguzi yatoa mapendekezo kwa serikali

    .

    Chanzo cha picha, IKULU

    • Kutenga siku ya maombelezi ya kitafa, kuwakumbuka Watanzania waliofariki kwenye ghasia za wakati na baada ya uchaguzi mkuu
    • Serikali iweke utaratibu kwa waliopata majeraha kupata usaidizi, ikiwemo viungo bandia
    • Serikali iweke mkakati wa kutoa huduma za kisaikolojia katika maeneo yaliyoathirika
    • Katiba mpya ipatikane ili itumike katika chaguzi zijazo
    • Kuunda tume ya maridhiano ya kitaifa katika nyanya za kijamii, kisiasa na kiuchumi
    • Kuundwe baraza la wazee ili kuisaidia tume ya maridhiano
    • Sheria ya tume huru ya uchaguzi itekelezwe kwa ukamilifu, ili kuondoa malamakio ya vya vya siasa kuhusu uhuru wa tume
    • Kuunda tume ya kijinai ili kuchunguza matukio ya jinai ya wakati wa vurugu za uchaguzi mkuu
    • Jeshi la polisi liunde utaratibu wa kurudisha mahusiano na wananchi
    • Serikali na vyombo dola vitekeleze majuku yake kwa kuzingatia uwazi na mfumo wa Kidemokrasia wa vyama vingi vya siasa
    • Maadili ya viongozi yasimamiwe, ili kudhibiti ufisadi na rushwa Baraza la vijana liundwe ili kuleta maridhiano na kushughulikia mambo ya vijana
  5. Haiwezekani mtu mwingine ambaye si Mtanzania awe na uchungu kuliko watanzania - rais Samia

    Rais Samia Suluhu Hassan amesema haiwezekani mtu mwingine ambaye si Mtanzania awe na uchungu kuliko watanzania.

    'Tunatamani siku zirudi nyuma, yaliyotokea Octoba 29 yasitokee'

    Akizungumza baada ya kusikiliza uwasilishwaji wa ripoti ya Tume ya uchunguzi wa matukio ya Oktoba 29 2025 rais Samia amevinyooshea kidole vyombo vya habari vya kimataifa kwa kufanya upotoshaji mkubwa kuhusu matukio ya oktoba 29.

    'Upotoshaji mkubwa ulifanywa na vyombo vya habari vya kimataifa'

    Aliyewapiganisha yuko nje anajifaidi. Tusikubali kuvurugwa. Aliongeza kusema Rais Samia. Tutakuwa tunajidanganya tusiposema ukweli kuwa yaliyotokea hayakututikisa.

    'Pendekezo la Tume tumelipokea na tutalifanyia kazi' alisisitiza Samia

  6. Sekta binafsi zapata hasara zaidi wakati wa vurugu

    Tume imebaini kutoka vyanzo mbali mbali kuwa mali za watu binafsi na serikali zilizoharbiwa zina thamani ya shilingi za Kitanzania 125 bilioni, mali za sekta binafasi au watu binafsi zina tahamai ya blioni 89. Na mali za umma au serikali ni shilingi bilioni 36.

    Tume imeeleza kuwa hasara kutokana na mali kuharibiwa na kuibiwa kutoka watu binafsi, inaweza kuwa kubwa zaidi kutokana na utunzaji duni wa kumbukumbu za biashara kwa baadhi ya watu.

  7. Madai ya uwepo wa makaburi ya halaiki hayana ushahidi – Tume

    Kuna taarifa kutoka kwa vyombo vya habari vya nje na mitandao ya kijamii juu ya uwepo wa makaburi ya halaiki katika eneo la Kondo Kunduchi, jijini Dar es Salaam.

    Tume ilitembelea eneo hilo na kupata taarifa kutoka kwa maafisa na kushirikisha watalaamu mbalimbali ili kufanya uchunguzi wa kisayansi.

    Uchunguzi wa tume umegundua kuwa madai ya uwepo wa makaburi ya halaiki hayawezi kuthibitishwa.

  8. Idadi ya majeruhi wa wakati wa vurugu yatajwa

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Hadi kufikia tarehe 31 Machi 2026, majeruhi waliokuwa wamehudumiwa katika vituo vya afya vya umma na binafsi walikuwa ni 2,390, kati yao raia ni 2,270 na maafisa na maaskari wa vyombo vya ulinzi na usalama 120.

    Kuna uwezekano kuwa wapo majeruhdi ambao hawako katika idadi hiyo, kwani kuna uwezekano baadhi ya majeruhi kupatiwa matibabu nje ya vituo vya afya na baadhi kukimbilia katika nchi jirani kwa kuogopa kukamatwa.

    Majeruhi waliopata majeraha makubwa ni 219. Kati yao majerahi 197 walikuwa na majeraha yanayotokana na risasi.

  9. Kuna madai ya watu kuuawa katika nyumba zao – Tume

    Tume imepokea madai kutoka kwa waathirika na mashahidi kuwa kuna watu waliuawa au kujeruhiwa katika maeneo ambayo hayakuwa na ghasia wala vurugu.

    Kuna madai ya watu kupigwa risasi katika nyumba makazi yao, ikiwa pamoja na ndani ya nyumba, sebuleni au ndani ya maduka.

    Hizi ni tuhuma nzito za uwezekano wa matumizi ya silaha nzito kinyume na sheria za kimataifa na kikanda.

  10. Idadi ya waliofariki inaweza kuwa kubwa zaidi

    .

    Tume imebaini kuwa kuna uwezekano kuwa badhi ya familia zimezika wapendwa wao bila kuwafikisha katika vituo vya kutolea huduma ya afya au hawakupata fursa ya kuja mbele ya tume.

    Tume pia inasema inawezekana kuwepo kwa majeruhu ambao walitbiwa nje ya mfumo rasmia na taarifa zao kutofikishwa katika vituo rasmia.

    Tume pia imepokea taarifa za watu kupotea au kutopatikna tangu wakati wa matukio ya vurugu za uchaguzi mkuu.

    Tume pia imepokea ushahidi kuwa watu 39 ambao familia ziliona miili ya wapendwa wao katika hospitali na vituo vya afya, na kutambuliwa lakini miili hiyo baadaye haikuonekana tena.

    Kwa kuzingantia hayo idadi ya vifo vya watu 518 inaweza kuwa sio idadi kamili ya waliofariki.

  11. 'Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni'

    Baadhi ya waathiriwa wa vurugu hizo waliopoteza wapendwa wao wameeleza hisia zao kwa BBC, wakisimulia maumivu, hofu na matumaini waliyonayo kufuatia tukio hilo.

    Mwanaume huyu tumehifadhi utambulisho wake alimpoteza kijana wake aliyefariki dunia kutokana na majeraha ya risasi aliyopata alipokuwa akitoka katika shughuli zake.'kijana wangu ameniachia mtoto mdogo' anayenitegemea.

    Kwa upande mwingine wake Mwanaume huyu anasema ripoti hii inamkumbusha machungu ya kumpoteza mke wake wa ndoa.'Nina wakati mgumu,tangu oktoba 30 nilimpoteza mke wangu wa ndoa'

    'Alipigwa risasi akiwa dukani kwake amekaa,nilimkuta ameshafariki dunia' alieleza. Wasamaria walinisaidia kumpeleka hospitali.Ripoti hii haina maana yoyote kwangu ikiwa hatutapata haki'.

  12. Tume ya uchunguzi yasema watu 518 walifariki dunia wakati wa ghasia za uchaguzi Tanzania

    Takriban watu 518 waliuawa wakati wa machafuko ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025 nchini Tanzania, tume ya uchunguzi ya serikali imebaini.

    Akizungumza katika Ikulu ya Tanzania jijini Dar es Salaam wakati akiwasilisha ripoti hiyo kwa Rais Samia Suluhu siku ya Alhamisi, Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji mstaafu Othman Chande, anasema idadi ya waliofariki inaweza kuwa kubwa kufuatia kuzikwa kwa baadhi ya wahanga bila taarifa kwa mamlaka.

    Chande anasema kuwa Akili Mnemba (AI) ilitumika kusambaza baadhi ya picha zinazoonyesha matokeo ya matukio hayo, ikiwa ni pamoja na madai ya maziko ya watu wengi.

    Hata hivyo alisema ushahidi wa kidijitali ni sehemu muhimu ya uchunguzi huo.

    Alieleza kuwa nyenzo hizo zilipatikana kutoka kwa mashuhuda na vyanzo vya wazi, vikiwemo vyombo vya habari na mitandao ya ki

    Dar es Salaam yaongoza kwa vifo wakati wa vurugu

    Huku idadi ya waliofariki wakati wa vurugu ikiwa ni watu 518, idadi ya waliofariki wanaume 490 sawa na asilimia 94.6, na wanawake 28, sawa na asilimia 5.4.

    Mkoa wa Dar es Salaam unaongoza kwa waliofariki ukiwa na vifo 182, Mwanza 90, Mbeya 80 na Arusha 53. Na 21 viikuwa vifo vya watoto. Na vifo 16 walikuwa askari na maafisa wa usalama.

  13. Tume yataja malengo ya walioshiriki katika vurugu

    Kuzuia uchaguzi: Lengo kuu ni kvurugu na kuzuia uchaguzi, lengo hili linathibitshwa na matukio mbali mbali, ikiwemo kushambulia askari, mawakala na wasimamizi wa uchaguzi, kuharibu mali za wasimamizi, vitisho, kuvamia vituo vya uchaguzi, kupora mali, kutishia waliojitokeza kupiga kura na waliopiga kura kukakwa au kujaribiwa kukatwa vidole.

    Kufikisha ujumbe: Tume inasema miongoni mwa walioshiriki katika vurugu ilikuwa ni kwa lengo la kufikisha ujumbe kwa serikali, tume inasema vijana walioshiriki walipata mwanya wa kufikisha ujumbe kwa serikali kuwa wanataka kusikilizwa.

    Wizi na uporaji: Miongoni mwa wafanya ghasia, walijitokeza makundi ya waliopora mali na kuiba. Uporaji ulitokea katika maduka na maeneo mengine ya biashara yaliyotembelewa na tume.

  14. Mbinu 16 zilitumika kufanikisha ghasia na vurugu - Tume

    Ripoti ya Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Oktoba 29, 2025, chini ya Mwenyekiti wa Tume, Jaji Mohamed Chande, amesema takaribani mbinu kumi na sita zilitumika wakati wa kutekeleza vurugu hizo.

    Akitaja baadhi ya mbinu hizo amesema, kuweka vizuiz barabarani, kuchoma moto, matumizi na ishara mbali mbali za kutambuliana, matumizi ya pikipiki, kufanya ghasia katika maeneno mengi kwa wakati mmoja.

  15. Tume yasema matukio ya vurugu yalifadhiliwa

    Tume imepata ushahidi kuwa matuko ya vurugu yalipangwa, yaliratibiwa, yalifadhiliwa na kutekelezwa na watu waliopata mafunzo.

    Waratibu walitumia mbinu mbalimbali, ikiwemo kuwasajili vijana.

    Tume hiyo inasema waratibu hao walikuwa wakizunguka maneno mbalimbali katika vyuo vikuu, masoko na vituo vya mabasi, na kuwaandikisha watu ili kushiriki katika ghasia za Oktoba 29.

    Tume inasema waratibu hawakumamatwa kwa sababu hawakuwepo wakati wa vurugu.

  16. Wanasiasa na Wanaharakati watajwa kuchochea vurugu Oktoba 29

    jm

    Chanzo cha picha, Reuters

    Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya wakati na baada ya uchaguzi wa Oktoba 29, Jaji Mohamed Chande, amesema kauli mbiu na matamko mbalimbali kutoka kwa baadhi ya wanasiasa na waharakati yalichochea vurugu, kwani walitumia changamoto za wananchi, kama fursa za kuwashawishi kushiriki ghasia hizo.

    Tume imebaini kulikuwa na vichocheo vikubwa vitatu vya kufanya ghasia:

    Mitandao ya kijamii: Amesema mitandao ilitumika kabla na baada ya uchaguzi mkuu, na wabuni mada ambao walihamasisha watu wasishiriki katika uchaguzi mkuu au kuhakikisha haufanyiki.

    Kauli mbiu: Amesema baadhi ya wanasiasa waliwahamasisha watu kufanya ghasia kwa kutumia kauli mbiu kama, "no reform no election, Oktoba hatutiki, Oktoba tunatoka, tumedhamiria uchaguzi hautofanyika, Samia Must Go, Tunataka kukomboa nchi yetu, hakuna uchaguzi chini ya serikali hii, tunahakikisha nchi haisimami, hakutakuwa na uchaguzi bila mabadiikio ya mfumo, serikali imepoteza uhalili, serikali iondoke, wagombea sio halali.

    Wanasiasa: Kundi la tatu la vichocheo, ni baadhi ya maeneo ya nchi ambapo wagombea wa viti vya udiwani na ubunge, ambao waliona ghasia zinawasaidia kudai mabadiliko ya mfumo na kupata wagombea ndani vya vyama vyao, nao waliwahamasisha wafuasi wao kufanya ghasia.

  17. 'Walinipa mchongo utakaonitoa kwenye umaskini' - shahidi

    Shahidi aliyefika mbele ya tume aliiambia Tume jinsi alivyopewa pesa ili kushiriki kwenye maandamano yaliyofuatia uchaguzi mkuu wa Tanzania.

    Kwa mujibu wa mwanyekiti wa Tume ya Kuchunguza Matukio ya Oktona 29 Othman Chande baathi ya wa waandamanaji walipewa hadi shi;ingi 10,000 za Tanzania kushiriki.

    Wizi na uporaji ulishuhudiwa baada ya makundi makubwa ya watu kujitokeza kuanza kuiba na kupora mali na kulikua ushahidi wa picha mjongea na mnato.

  18. Hayakuwa maandamano ya amani bali ghasia- Jaji Chande

    Tume imehitimisha kuwa maandamano yaliyofanyika hayakuwa ya amani bali ghasia kinyume cha katiba na sheria.

    Ni haki ya kikatiba ya kila mtu kupiga kura, ghasia zilipangwa na kutekelezwa siku ya kutekeleza haki ya kikatiba ya wananchi kupiga kura.

    Hitimisho la tume kilichotokea siku ya uchaguzi mkuu, haikua maandamano ya amani bali ghasia, hayakuzingatia matakwa ya katiba na sheria za nchi

  19. Waandamanaji walipewa simu- Jaji Chande

    Matumizi ya mitandao ya kijamii, waliibuka wabuni mada kwenye mitandao, ikiwemo mada za kutoshiriki uchaguzi mkuu, na kupanga mbinu na kuwaelekeza waliokubali vurugu.

    Walioshiriki kufanya ghasia, waliokuja mbele ya tume, walipewa simu za mkononi na kupiga picha za maeneo mbalimbali ya ghasia na kurusha moja kwa moja kwenye mitandao ya kijamii ili kuibua hasira kwa wananchi, na waliaminishwa jeshi la Tanzania lipo upanda wao. anaendelea kusema Mwenyetkiti wa Tume Othman Chande.

  20. Vyanzo vya ghasia: Tume yabainisha vyanzo vitano na vichocheo

    Jaji Chande ametaja sababu za kisiasa ,ikiwemo madai ya Tume huru ya uchaguzi, changamoto za kiuchumi ajira ugumu wa maisha, kijamii kama vile kukosekana kwa uzalendo kuwa miongoni mwa vyanzo vya ghasia za uchaguzi wa Oktoba 29.

    Kwanza: Masuala ya kisasa ikiwemo madai ya katiba mpya, maboresho ya tume huru ya uchaguzi

    Pili: Masuala ya kijamii, ukosefu wa ajira, maisha magumu na mazingira ya kibiashara, utitiri wa kodi

    Tatu: masuala ya kijamii yanayohusisha mmonyoko wa maadili na kukosa uzalendo na kutokushughuliwa kwa madai ya rushwa, kupotea na kutekwa kwa watu

    Nne: Utendaji wa wafayakazi wa umma-

    Tano: Uhusiano wa kimataifa - Tume inasema kumekuwa na mkakati wa jamiiya kimataifa kuingilia maswala ya ndani ya Tanzania