Mfalme Charles III kuhutubia bunge la Congress nchini Marekani

Chanzo cha picha, PA Media
Hii leo ni siku ya pili ya ziara ya siku nne ya Mfalme Charles III na Malkia Camilla nchini Marekani.
Wafalme hao watahudhuria hafla ya kijeshi katika ikulu ya White House kabla ya kufanya mkutano na Rais wa taifa hilo Donald Trump.
Mfalme Charles III, anatarajiwa kuandikisha historia, kuwa kiongozi wa pili wa kifalme kutoka Uingereza kulihutubia bunge la Marekani la Congress, baada ya mamayake Malkia Elizabeth II, kufanya hivyo mwaka wa 1991.
Hotuba ya mfalme Charles III inatarajiwa kusema kuwa “mara kwa mara nchi zetu mbili zimekuwa zikipata njia za kuja pamoja na kushirikiana”
Ziara ya Mfalme Charles III, inajiri wakati kumekuwa na mvutano kati ya Uingereza na Marekani kuhusu vita vya Iran, na inatarajiwa kuwa ziara ya mfalme itasaidia kutatua mvutano huo na kurekebisha uhusiano wa Waziri mkuu wa Uingereza Keir Starmer na Donald Trump.
Kwa picha: Mfalme Charles III na Malkia Camilla walipowasili nchini Marekani

Chanzo cha picha, Getty Images

Chanzo cha picha, Getty Images

Chanzo cha picha, Getty Images

Chanzo cha picha, Getty Images
Pia unaweza kusoma:












