Tetesi za soka Ulaya: PSG yajiunga na Arsenal kumwinda Gibbs-White
Arsenal F.C. huenda ikakumbana na ushindani mkali kutoka kwa Paris Saint-Germain katika harakati za kumsajili kiungo mshambuliaji wa Nottingham Forest F.C., Morgan Gibbs-White.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 yuko kwenye orodha ya Arsenal kama mbadala anayetarajiwa wa nyota wa Aston Villa F.C., Morgan Rogers, mwenye umri wa miaka 23.
Hata hivyo, PSG pia inafuatilia kwa karibu hali yake.
Wakati huo huo, inaelezwa kuwa winga wa Georgia wa PSG, Khvicha Kvaratskhelia, ndiye mchezaji ambaye rais wa Real Madrid C.F., Florentino Pérez, anapanga kumsajili iwapo atashinda uchaguzi wa urais wa klabu hiyo. (Teamtalk).
Kocha mpya wa Real Madrid, José Mourinho, naye anaripotiwa kutaka huduma za kiungo wa Ureno Bernardo Silva baada ya nyota huyo kuondoka Manchester City F.C. mwishoni mwa msimu. (AS - in Spanish)
Kwa upande mwingine, wakala wa Jürgen Klopp amesema Mjerumani huyo hana mpango wa kurejea kufundisha klabu yoyote kwa sasa, baada ya mgombea wa urais wa Real Madrid, Enrique Riquelme, kudai angejaribu kumshawishi kujiunga na klabu hiyo endapo angechaguliwa. (Sky sports-Germany)
Tottenham Hotspur F.C. bado ina nia ya kumsajili winga wa Brazil Savinho. Inadaiwa mchezaji huyo mwenye miaka 22 yuko tayari kushinikiza uhamisho huo baada ya Manchester City kukataa ofa ya Spurs msimu uliopita. (Mirror).
Mshambuliaji wa Italia Federico Chiesa amesema anahitaji kupata muda zaidi wa kucheza akiwa Liverpool na atazungumza na kocha mpya wa Reds, Andoni Iraola, kabla ya kufanya uamuzi kuhusu mustakabali wake. (Gazzetta dello Sport - in Italian)
Liverpool pia haina mpango wa kumuuza winga chipukizi wa England Rio Ngumoha mwenye miaka 17, licha ya taarifa kwamba FC Bayern Munich inamfuatilia kwa ajili ya usajili wa majira ya joto.(Sky Sports)
Kwingineko, winga wa Newcastle United F.C., Harvey Barnes, ameibuka kulengwa kusajiliwa na Aston Villa. (Football Insider)
Nazo Leeds United F.C. na Ipswich Town F.C. zinashindania saini ya kipa wa England Nick Pope kutoka Newcastle. (Sun)
Aidha, kocha Russell Martin yuko katika mazungumzo ya hatua za mwisho na Leicester City F.C. huku akitafakari kurejea kwenye ukocha. (Telegraph - subscription required)
Pia unaweza kusoma: