Álvarez kutua Arsenal?
Uhamisho wa mshambuliaji wa Atletico Madrid, Julián Álvarez, unaweza kuwa miongoni mwa dili kubwa zaidi za siku ya mwisho ya usajili leo, huku hatima yake ikiwa bado haijajulikana.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 anataka kuondoka Atletico, lakini klabu hiyo imekataa kumuuza kwenda Barcelona.
Hata hivyo, Atletico iko tayari kufanya biashara na Arsenal, ambayo imekuwa ikimfuatilia Álvarez kwa muda mrefu.
Arsenal imekuwa ikifuatilia kwa karibu hali hiyo huku Atletico ikitaka kumuuza mchezaji huyo kuwa euro milioni 150, sawa na takriban pauni milioni 128.
Álvarez hakufanya mazoezi siku kadhaa na hakusafiri na kikosi cha Atletico kilichoikabili Sevilla Jumamosi.
Kocha Diego Simeone alisema mchezaji huyo hakuwa katika hali nzuri ya kutosha kusafiri.
Hata hivyo, Simeone amejaribu kutuliza hali hiyo, akisema atafanya kila awezalo kumfanya Álvarez ajisikie kuwa sehemu muhimu ya kikosi atakaporejea mazoezini.