Marekani inaendelea na Mazungumzo na Iran huku mashambulizi yakisitishwa - Trump

Hata hivyo, ameonya kuwa iwapo mazungumzo hayo hayatakuwa na mafanikio, Marekani "itarejea kufanya kile tulichokuwa tukifanya" kabla ya kusitishwa kwa mashambulizi.

Muhtasari

Ruka Video uendelee
  • .
  • xx
  • xx
  • xx
  • Lungu
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • xx
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Asha Juma

  1. Johnson & Johnson yajitolea kulipa hadi $5.5bn kumaliza kesi za poda ya watoto

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Kampuni ya Johnson & Johnson (J&J) imejitolea kulipa hadi dola bilioni 5.5 (pauni bilioni 4.14) ili kumaliza maelfu ya kesi zinazodai poda yake ya watoto pamoja na bidhaa nyingine zenye madini ya talcum husababisha saratani ya ovari au kifuko cha mayai.

    Makubaliano hayo makubwa yanakusudia kumaliza mzozo wa kisheria uliodumu kwa miaka kadhaa na kuendelea kuigharimu kampuni hiyo kubwa ya huduma za afya nchini Marekani.

    J&J imeendelea kusisitiza kuwa bidhaa zake zenye talcum hazisababishi saratani, na tayari imebadilisha viambato vya poda yake ya watoto inayotumiwa na watu wengi.

    Makamu wa Rais wa masuala ya kesi za kisheria wa kampuni hiyo, Erik Haas, alisema Jumatatu kuwa madai hayo "hayana msingi", na kwamba J&J imeamua kufikia makubaliano ili kutatua kabisa suala hilo.

    Kampuni hiyo imesema makubaliano hayo yatahusisha takriban kesi 69,000, ambazo ni sehemu kubwa ya madai yaliyosalia yanayohusiana na bidhaa za talcum. J&J imeeleza kuwa italipa hadi dola bilioni 3 mwaka ujao, na kusitarajiwe malipo mengine kabla ya mwaka 2028.

    J&J pia imesema pendekezo hilo litalazimika kukubaliwa na kampuni za mawakili zinazowawakilisha asilimia 95 ya walalamishi wa kesi za saratani ya ovari katika mahakama za majimbo na za shirikisho, kabla ya makubaliano hayo kukamilika.

    Katika taarifa yake, Haas alisema kampuni ina imani kuwa ingeibuka mshindi endapo kesi hizo zingeendelea mahakamani, kama ilivyofanikiwa katika kesi nyingi ambazo tayari zimeamuliwa.

    Aliongeza kuwa makubaliano hayo yataiwezesha kampuni kuhitimisha suala hilo na kuelekeza nguvu zake katika jukumu lake la kutengeneza dawa na vifaa vya tiba vinavyookoa maisha.

    Soma Zaidi:

  2. Mazungumzo ya vita vya Iran yanaendelea huku mashambulizi yakisitishwa - Trump

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema kuwa kuna "mazungumzo ya kirafiki yanayoendelea" kuhusu mzozo wa Iran, baada ya pande zinazopigana kutoshambuliana kwa siku ya tatu mfululizo.

    Akiwa ndani ya ndege ya Air Force One siku ya Jumatatu, Trump alieleza matumaini yake kwamba vita hivyo vinaweza kufikia mwisho. Aliwaambia waandishi wa habari: "Ninaamini kuna uwezekano mkubwa jambo fulani likatokea."

    Alionyesha matumaini kwamba vita vinaweza kumalizika Jumatatu, akiwaambia waandishi wa habari ndani ya ndege ya Air Force One: "Nafikiri kuna fursa nzuri ya kutokea kwa jambo fulani."

    Hata hivyo, alionya kuwa iwapo mazungumzo hayo hayatakuwa na mafanikio, Washington "itarejea kufanya kile tulichokuwa tukifanya" kabla ya kusitishwa kwa mashambulizi.

    Kwa upande wake, Tehran imekanusha kuwa kuna mazungumzo yoyote ya moja kwa moja yanayoendelea.

    Trump alisema aliamua kusitisha mashambulizi ya Marekani dhidi ya Iran siku ya Ijumaa baada ya nchi zinazosaidia kupatanisha pande hizo kumwomba kutoa fursa nyingine kwa mazungumzo.

    Iran pia imesitisha mashambulizi yake.

    Hatua hiyo inafuatia karibu wiki mbili za mashambulizi ya kila siku ya Marekani na ya kulipizana kisasi kati ya pande hizo, hali iliyovuruga kwa kiasi kikubwa makubaliano ya usitishaji mapigano yaliyofikiwa mnamo mwezi Juni.

    Wakati huo, jeshi la Marekani lilisema mashambulizi yake yalilenga kupunguza uwezo wa Iran wa kuhatarisha usafirishaji wa meli za kibiashara katika Mlango Bahari wa Hormuz, ambao ni njia muhimu duniani ya usafirishaji wa mafuta.

    Soma Zaidi Hapa:

  3. Hujambo Msomaji wetu. Karibu katika matangazo yetu mubashara tarehe ni 28/07/2026.