Iraq yaitaka Saudia kumuondoa balozi wake

Chanzo cha picha, AFP
Iliyochapishwa
Wizara ya mashauri ya nchi za nje ya Iraq, imeiomba Saudi Arabia imuondoe balozi wake mjini Baghdad.
Wanasiasa wa Ki-Shia wamesema mara kadha, kwamba bwana Thamer al-Sabhan aondoshwe, baada ya matamshi ya balozi huyo, juu ya kuhusika kwa Iran nchini Iraq, akidai kuwa wanamgambo wa Ki -Shia, wanazidisha mvutano na Sunni.
Juma lilopita, wakuu wa Iraq walikanusha ripoti za vyombo vya habari, kwamba kuna njama ya kumuuwa balozi huyo.








