Moja kwa moja, Marekani yaishambulia tena Iran, Tehran yajibu

Marekani imedai kuzuia mashambulizi ya Iran baada ya kudungua makombora ya balistiki na ndege zisizo na rubani zilizokuwa zikielekea Mlango wa Hormuz pamoja na nchi jirani za Ghuba ya Uajemi.

Muhtasari

Marekani yaishambulia tena Iran, Tehran yajibu

Moja kwa moja

Na Beldeen Waliaula

  1. Marekani yaishambulia tena Iran, Tehran yajibu

    AFP

    Chanzo cha picha, AFP

    Jeshi la Marekani limesema limedungua ndege nne zisizo na rubani za Iran zilizokuwa zikielekea Mlango bahari wa Hormuz, na kudai kuwa yalikuwa tishio la moja kwa moja kwa usafiri wa majini eneo hilo na mataifa mengine ya Ghuba ya Uajemi.

    Kituo kikuu cha kuendesha oparesheni za Marekani za Kijeshi (CENTCOM) imesema kuwa baada ya kudungua ndege hizo, vikosi vya Marekani vilishambulia vituo vya rada za ufuatiliaji vya Iran katika eneo la Goruk na Kisiwa cha Qeshm ili kuzuia mashambulizi zaidi.

    Iran ilijibu hatua ya Marekani kwa kurusha makombora ya balistiki na kulenga kambi za kijeshi za Marekani zilizoko Kuwait na Bahrain.

    CENTCOM imesema kati ya makombora saba ya Iran yaliyolenga nchi hizo mbili za Ghuba, sita yalidunguliwa huku moja haikufikia lengo lake.

    Pia unaweza kusoma:

  2. Hujambo na karibu katika matangazo yetu ya moja kwa moja