Marekani yaishambulia tena Iran, Tehran yajibu

Chanzo cha picha, AFP
Jeshi la Marekani limesema limedungua ndege nne zisizo na rubani za Iran zilizokuwa zikielekea Mlango bahari wa Hormuz, na kudai kuwa yalikuwa tishio la moja kwa moja kwa usafiri wa majini eneo hilo na mataifa mengine ya Ghuba ya Uajemi.
Kituo kikuu cha kuendesha oparesheni za Marekani za Kijeshi (CENTCOM) imesema kuwa baada ya kudungua ndege hizo, vikosi vya Marekani vilishambulia vituo vya rada za ufuatiliaji vya Iran katika eneo la Goruk na Kisiwa cha Qeshm ili kuzuia mashambulizi zaidi.
Iran ilijibu hatua ya Marekani kwa kurusha makombora ya balistiki na kulenga kambi za kijeshi za Marekani zilizoko Kuwait na Bahrain.
CENTCOM imesema kati ya makombora saba ya Iran yaliyolenga nchi hizo mbili za Ghuba, sita yalidunguliwa huku moja haikufikia lengo lake.
Pia unaweza kusoma:
