Waasi wa Houthi 'wadhibiti' Kisiwa cha Perim - ripoti
Waasi wa Houthi wamedhibiti Kisiwa cha Perim katika Mlango-bahari wa Bab al-Mandab, kulingana na chanzo cha habari.
Awali, tuliripoti kuwa kundi hilo lilikuwa limefika katika kisiwa hicho muhimu.
Shirika la habari la AFP pia linasema kuwa Wahouthi wameteka Kisiwa cha Perim, ambacho pia hujulikana kama Mayyun, kulingana na mashuhuda na afisa wa serikali ya eneo hilo.
"Boti zilizobeba wapiganaji wenye silaha wa Houthi zilifika Kisiwa cha Mayyun baada ya vikosi vya serikali kuondoka hapo jana," afisa huyo aliambia AFP.
Huku hayo yakijiri, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani ameiambia BBC kwamba Marekani iko katika mawasiliano ya mara kwa mara na washirika wake wa kikanda kuhusu Yemen na bado inaendelea kuzingatia malengo yake ya kupambana na ugaidi dhidi ya Wahouthi.
Taarifa hiyo inasema kuwa maslahi muhimu ya Marekani katika Mashariki ya Kati ni pamoja na kulinda uhuru wa usafiri wa meli katika Bahari Nyekundu na ukanda huo, pamoja na kuzuia usafirishaji wa ugaidi.
Aidha, imeeleza kuwa utawala wa Trump umeonyesha wazi dhamira yake ya kutetea maslahi hayo dhidi ya vitendo vya uchokozi vya Iran na makundi yanayoiunga mkono.
Hata hivyo, Wizara ya Mambo ya Nje haikutoa maelezo zaidi kuhusu hatua za karibuni za Wahouthi wanaoungwa mkono na Iran za kusonga mbele kuelekea maeneo muhimu ya bandari.
Unaweza kusoma;