Tumeondoa mabomu yote ya baharini katika Mlango wa Hormuz - Trump
Rais wa Marekani Donald Trump amesema Jeshi la Wanamaji la Marekani limeondoa na kulipua mabomu yote ya baharini katika Mlango Bahari wa Hormuz,ambayo ni njia muhimu ya majini ambayo Iran kwa kiasi kikubwa imeifunga tangu kuanza kwa vita Mashariki ya Kati.
“Iran imearifiwa kwamba meli au boti yoyote itakayoweka mabomu mapya ya baharini itaharibiwa mara moja,” Trump alisema kupitia mtandao wake wa Truth Social.
Iran haijatoa maoni kuhusu madai hayo.
Kufungwa kwa Mlango huo kumesababisha kupanda kwa bei ya mafuta katika masoko ya dunia. Trump amekuwa akisema mara kwa mara kwamba Marekani inadhibiti eneo hilo, huku Iran ikifyatulia risasi meli zilizojaribu kuvuka bila idhini yake.
Soma pia: