Moja kwa moja, Trump na maafisa wake 'huenda' ndio walengwa wa shambulio la risasi Washington - Mamlaka

Mshukiwa anatarajiwa kushtakiwa kwa makosa ya kutumia silaha katika uhalifu wa vurugu pamoja na kushambulia maafisa wa serikali kwa kutumia silaha hatari.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Ambia Hirsi

  1. 'Tunaishi katika ulimwengu wa ajabu' - asema Trump baada ya jaribio la mauaji dhidi yake

    .

    Chanzo cha picha, reu

    Tukio la shambulio la risasi kwenye dhdifa ya Waandishi wa White House linaonekana kuwa jaribio la tatu la mauaji dhidi ya Donald Trump, kufuatia matukio ya Butler, Pennsylvania mnamo Julai 2024, na katika klabu yake ya gofu huko Florida mnamo Septemba mwaka huo.

    Lakini katika mahojiano na 60 Minutes jana, Trump alisema: "Sikuwa na wasiwasi. Ninaelewa maisha. Tunaishi katika ulimwengu wa ajabu."

    Alipoulizwa kuhusu kilichojiri - ambapo JD Vance aliondolewa wa kwanza ukumbini - Trump alisema "haikuwa rahisi" kwa maafisa wa usalama kumuondoa kwenye chumba hicho.

    "Nilitaka kuona kinachofanyika.. nilitaka kuona kinachoendelea. Na kufikia wakati huo ndipo tulibaini, labda kuna kitu kibaya kimetokea."

    Alipoulizwa kuhusu "kushuka" alipokuwa akiongozwa kutoka ukumbini, Trump alijibu: "Nilianza kutembea nao [maafisa wa usalama]. Niligeuka, nikaanza kutembea, wakasema, 'Tafadhali shuka. Tafadhali shuka chini.'

    "Kwa hiyo nilishuka na yule mwanamke wa kwanza akashuka pia."

    CBS, mshirika wa habari wa BBC imeona hati iliyoandikwa inayoaminika kuhusishwa na mshukiwa, Cole Allen, ikisema alitaka kuwalenga wanachama wa utawala wa Trump "kutoka ngazi ya juu hadi chini".

    Wakati wa mahojiano ya Dakika 60, Trump alikasirishwa na mwandishi wa habari Norah O'Donnell baada ya kuuliza juu ya yaliyomo kwenye dondoo, ambayo ni yalijumuisha maneno kama vile "mnyanyasaji, mbakaji na msaliti".

    Alimsuta O'Donnell kwa kumuuliza juu ya dondoo hizo, na kuongeza kuwa "unapaswa kuona aibu kusema hivyo, kwa sababu mimi sihusiki na mambo hayo".

    Maelezo zaidi:

  2. Bei ya mafuta yapanda baada ya mazungumzo ya amani ya Marekani na Iran kukwama

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Bei ya mafuta imepanda baada ya duru ya pili ya mazungumzo ya amani kati ya Marekani na Iran kukwama tena.

    Mafuta ya Brent ilipanda hadi dola 107.26 kwa pipa, wakati mafuta yasiyosafishwa ya Marekani yalipanda kwa 1% kwa dola 95.40.

    Haya yanajiri baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema Jumamosi kwamba Washington iliahirisha mpango wa kutuma ujumbe wake nchini Pakistan kwa mazungumzo na wenzao wa Iran.

    Ugavi wa nishati duniani umekuwa chini ya shinikizo kubwa tangu kuanza kwa vita vya Iran kwani njia kuu ya baharini ya Hormuz imefungwa.

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Seyed Abbas Araghchi alisema Jumapili kwamba "majadiliano muhimu juu ya masuala ya nchi mbili na maendeleo ya kikanda" yanaendelea na Oman.

    Alichapisha kwenye mtandao wa kijamii: "Lengo letu lilijumuisha njia za kuhakikisha usafiri salama ambao ni wa kufaidisha majirani wote wapendwa na ulimwengu.

    Majirani zetu ndio kipaumbele chetu." Araghchi amewasili St Petersburg, Urusi leo Jumatatu "kwa lengo la kukutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Urusi Vladimir Putin", shirika la habari la serikali ya Iran Irna liliripoti.

    Takriban thuluthi moja ya mafuta ghafi na gesi asilia (LNG) hupitia Mlango-Bahari wa Hormuz.

    Maelzo zaidi:

  3. Vita vya Iran: Araqchi awasili Urusi kwa mazungumzo na Putin

    Putin na Araqchi

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araqchi amewasili St. Petersburg, Urusi ambapo anatarajiwa kukutana na Rais wa Urusi Vladimir Putin mjini Moscow, shirika la habari la Iran, limeripoti likimnukuu balozi wa Iran nchini Urusi, Kazem Jalali.

    Bwana Araghchi alisafiri kwa ndege ya "Minab Flight 168" kuwakumbuka watoto waliouawa katika shule ya Minab, Mkoa wa Hormozgan, waliouawa katika shambulio la Marekani na Israel dhidi ya Iran.

    Madhumuni ya ziara ya Bw. Araqchi inaelezwa kuwa "kukutana na kujadiliana na Rais wa Urusi Vladimir Putin."

    .

    Chanzo cha picha, TELEGRAM/REUTERS

    Siku ya Jumapili, baada ya kusafiri hadi Muscat na kukutana na maafisa wa Oman, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran alielekea Islamabad kwa mara ya pili katika siku tatu zilizopita, na kukutana na maafisa wa Pakistan kabla ya kuondoka kwenda Moscow.

    Maelezo ya ziara hizi na sababu ya kurejea kwake Oman na Pakistan bado haijafichuliwa.

    Pia unaweza kusoma:

  4. Watu 14 wauawa Lebanon licha ya mpango wa usitishaji mapigano kufikiwa

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Wizara ya Afya ya Lebanon inasema kuwa watu 14 wakiwemo watoto wawili waliuawa Jumapili katika mashambulizi ya Israel.

    Msemaji wa Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) hapo awali alitoa ilani ya kuhama kwa wakaazi kutoka vijiji kadhaa kusini mwa Lebanon, na kuonya kuwa wa kupuuza ilani hiyo "kungelihatarisha maisha yao".

    IDF baadaye ilisema ilifanya "mashambulizi ya angani" kuwalenga wanamgambo wa Hezbollah katika maeneo ya kusini mwa Lebanon ambayo inadai yanatumiwa "kuendeleza mashambulizi dhidi ya wanajeshiwa Israel".

    Pia imesema mwanajeshi wa IDF mwenye umri wa miaka 19 ameuawa na wengine sita kujeruhiwa na shambulio la ndege isiyo na rubani ya Hezbollah nchini Lebanon.

    Hezbollah ilirusha ndege tatu zisizo na rubani kuelekea Israeli, IDF iliripoti, huku ikiongeza kuwa ziliangushwa na jeshi la anga la Israeli kabla ya kuvuka mpaka.

    Nchi hizo mbili zilifikia mpango wa usitishaji mapigano, ambao ulianza kutekelezwa tarehe 16 Aprili na kuongezwa muda kwa wiki tatu Alhamisi wiki iliyopita.

    Chini ya makubaliano hayo, Israel inasalia na "haki yake ya kuchukua hatua zote za kujilinda, wakati wowote, dhidi ya mashambulizi yaliyopangwa, yanayokaribia, au yanayoendelea".

    Akizungumza katika mkutano wa serikali, Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alisema IDF "inaendelea, na inafanya kazi kwa nguvu" nchini Lebanon, akisema hatua za Hezbollah "zinasambaratisha usitishaji mapigano".

    Soma zaidi:

  5. Traoré alaani mashambulizi ya Mali na kuyataja kuwa 'ya kinyama'

    Kapteni Ibrahim Traoré

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Kapteni Ibrahim Traoré, rais wa muungano wa Mataifa ya Sahel (AES), amelaani mashambulizi ya kupangwa nchi ya Mali, takribani saa 48 baada ya matukio hayo.

    Katika taarifa iliyotolewa Jumapili usiku, alitaja mashambulizi hayo kama "ya kinyama " na kusema "yanaungwa mkono na maadui wa mapambano ya ukombozi wa Sahel".

    Traoré aliongeza kuwa mashambulizi hayawezi "kuyumbisha nia ya watu mashujaa wa Sahel kuishi kwa uhuru, amani na heshima". Pia alitoa salamu za rambirambi kwa walioathirika.

    Alisema mashambulizi hayo yaliyoratibiwa yalipangwa kwa muda mrefu kwa madhumuni ya kuathiri vikosi vya usalama vya Mali na kuwatia hofu raia.

    Kapteni Traoré alichukua urais wa zamu wa AES mwezi Desemba, akichukua nafasi ya kiongozi wa kijeshi wa Mali, Jenerali Assimi Goïta.

    AES inayaleta pamoja mataifa ya Mali, Niger na Burkina Faso, ambayo yanaongozwa na serikali za kijeshi zilizoingia madarakani kufuatia mapinduzi katika miaka ya hivi karibuni.

    Nchi hizo tatu zilijiondoa katika Jumuiya ya kikanda ya Ecowas na tangu wakati huo zimeimarisha ushirikiano chini ya muungano huo.

    Ubia huo unalenga kuimarisha uratibu wa usalama, kuunganisha rasilimali na kukuza utangamano wa kiuchumi, ikijumuisha mipango ya miundomsingi ya pamoja, usafiri huria wa watu, na, kwa muda mrefu, soko la pamoja na sarafu.

    Soam pia:

  6. Trump na maafisa wake 'huenda' ndio walengwa wa shambulio la risasi Washington - Mamlaka

    Trump

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Rais wa Marekani Donald Trump na maafisa wake ndio "huenda" walengwa wa mtu anayeshukiwa kuwa na bunduki ambaye alijaribu kuvamia dhifa ya Waandishi wa White House, kaimu Mwanasheria Mkuu wa Marekani Todd Blanche amesema.

    Mshukiwa huyo, aliyetambuliwa na vyombo vya habari vya Marekani kama Cole Tomas Allen mwenye umri wa miaka 31, alikamatwa baada ya polisi kusema alifyatua risasi karibu na kituo cha ukaguzi wakati wa tukio katika hoteli ya Washington DC siku ya Jumamosi.

    Blanche, akizungumza na NBC News, alisema nia ya mtu anayedaiwa kuwa na bunduki bado inachunguzwa, lakini matokeo ya "awali" yanaonyesha kuwa alikuwa akiwalenga maafisa wa utawala.

    Kikosi kazi cha FBI cha kitengo cha uhalifu na ugaidi kinachunguza tukio hilo.

    Baada ya kuondolewa jukwaani na kupelekwa mahali salama, Trump baadaye aliwaambia waandishi wa habari katika kikao fupi siku ya Jumamosi: "Nadhani hakuna taaluma ambayo ni hatari zaidi".

    Katika taarifa ya Jumapili, Ikulu ya White House ilisema Trump "yuko imara" baada ya kunusurika, pamoja na wajumbe wa baraza la mawaziri, "jaribio la mauaji wakati risasi zilifyatuliwa".

    Rais wa Chama cha Waandishi wa Habari wa Ikulu ya White House, Weijia Jiang, alitaja shambulio hilo kuwa "la kutisha".

    Maelezo zaidi:

  7. Natumai hujambo. Karibu kwa matangazo ya moja kwa moja leo Jumatatu 27.04.2026