Mshukiwa Essa Suleiman ashtakiwa kwa jaribio la mauaji baada ya Wayahudi wawili kuchomwa kisu Uingereza

Chanzo cha picha, EPA
Essa Suleiman amefunguliwa mashtaka ya jaribio la mauaji baada ya wanaume wawili wa Kiyahudi kuchomwa kisu Golders Green, kaskazini mwa London, Polisi wa Metropolitan wamesema.
Kijana huyo mwenye umri wa miaka 45 ameshtakiwa kwa makosa mawili ya kujaribu kuua na shtaka moja la kupatikana na kifaa chenye ncha kali katika eneo la umma kuhusiana na tukio hilo la Jumatano.
Pia ameshtakiwa kwa jaribio la mauaji kuhusiana na tukio tofauti katika mtaa wa Great Dover huko Southwark mapema siku hiyo hiyo.
Siku ya Alhamisi, kiwango cha tishio la ugaidi nchini Uingereza kilipandishwa kufuatia shambuliwa la kisu dhdi ya wanaume wawili wa Kiyahudi.
Serikali inasema kuwa kupandishwa kwa kiwango cha tishio hakukutokana tu na shambulio la Golders Green, bali pia kumechochewa na “ongezeko la vitisho vya kijihadi na vya mrengo mkali wa kulia.”
Kamishna Mark Rowley atazungumza kwenye Kiamsha kinywa cha BBC asubuhi ya leo kuhusu tukio hilo. Tutakuwa tunakuletea sasisho zote za hivi punde hapa.
Maelezo zaidi:







