Rais Ruto amzawadia mwanariadha wa Kenya Sabastian Sawe

Chanzo cha picha, IKULU
Rais wa Kenya William Ruto leo amemzawadia shujaa wa mbio za marathon Sebastian Sawe gari jipya alilochagua likiwa na nambari maalum zilizo na muda wake wa kuvunja rekodi wa mbio za marathon 1:59:30 pamoja na pesa taslimu takriban £45,000 (Shilingi milioni 8 za Kenya) kama utambulisho wa mafanikio yake ya kihistoria katika riadha.
Sawe mwenye umri wa miaka 30 aliyeandikisha historia katika mbio za Marathon ya London tarehe 26 April kwa kuandikisha muda wa saa 1.59.30, alituzwa shilingi milioni 8 za Kenya kwa ushindi huo na pia ametakiwa kuchaguwa gari la chaguo lake litakalonunuliwa na Rais Ruto.
Sawe alikabidhiwa nambari ya usajili wa gari iliyoandkiwa 1.59.30 akielezwa kuwa ni ishara ya gari lolote alitakalo atanunuliwa na Rais kama bahshishi
Mbali na fedha kutoka kwa Rais, Mwanariadha huyo pia alivuna shilingi milioni 7.1 kutoka kwa usimamizi wa London Marathon kwa kuvunja rekodi ya mbo hizo na isitoshe na marupuru ya shilingi milioni 42.3.
Inakadariwa akichanganya na fedha za malipo ya biashara kwa ushirikiano wake na kampuni ya michezo ya adidas, huenda Sawe akakusanya jumla ya shilingi milioni 129 za Kenya kwa ufanisi wake.
Rais Ruto alisifu nidhamu na azma ya Sawe, akielezea utendakazi wake kama wakati wa fahari ya kitaifa ambayo inaimarisha ubabe wa Kenya katika mbio za masafa marefu.
Kwa furaha na bashasha mwanariadha huyo aliyetekwa na hisia nyingi za furaha alikosa maneno ya kujieleza huku akiahidi kuwa atazidi kushamiri katika riadha hizo akilenga kuendelea kuipaisha bendera ya Kenya katika riadha za kimataifa.
‘'Asante sana Rais Ruto kwa ualishi huu,nashkuru kupata fursa hii ya kuiwakilisha Kenya,naahidi kuwa huu ni mwanzo nitajia juhudi nizidi kufanya vyema na kushinda dhahabu,'’alisema Sawe
Kutokana na ufanisi huo,Rais William Ruto ameahidi kuwa serikali yake itawapa fedha maalum washindi wote wa riadha watakaowakilisha Kenya katika mashindano ya kimataifa.Alisema‘
Mshindi wa dhahabu tutampa shilingi milioni tatu, fedha milioni mbili na shaba milioni moja ili kwapa motisha wa talanta zao na pia kuwawezesha kimaendeleo ya maisha,’'alimaliza.
Waziri wa michezo nchini Kenya Salim Mvurya amesema Serikali itaboresha maslahi ya wanamichezo nchini kwa kuwekeza katika miundo mbinu sahihi ikiwemo viwanja.
Sebastian Sawe alianza kushiriki kwenye riadha za Maradhon mwaka 2024 tu akishinda marathon ya Valencia kwa muda wa saa 2.2.05.
Mashindano ya Marathon ya London ni marathon yake ya nne tu kushiriki na amefanikiwa kweka rekodi ya dunia .








