Moja kwa moja, Mashambulizi yasitishwa: Trump aitaka Iran kufanya makubaliano haraka

Trump amesema uamuzi huo ulifikiwa kwa ushirikiano na Israel.

Muhtasari

Ruka Video uendelee
  • xx
  • Besigye
  • .
  • xx
  • xx
  • xx
  • Lungu
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • xx

Moja kwa moja

Na Asha Juma

  1. Uganda yafanikiwa kudhibiti Ebola huku DRC ikiendelea kupambana na mlipuko huo hatari

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Uganda imefanikiwa kudhibiti Ebola na kwa sasa haina maambukizi ya ugonjwa huo, huku hali ikiwa tofauti nchini DRC ambako mlipuko unaendelea kuenea na idadi ya vifo vilivyothibitishwa ikizidi 1,500.

    Maafisa wa afya nchini Uganda wanasema mafanikio hayo yametokana na utambuzi wa haraka wa wagonjwa, ufuatiliaji wa waliokutana na maambukizi, pamoja na kuweka wagonjwa kwenye vituo maalum vya matibabu kabla ya ugonjwa kusambaa kwenye jamii.

    Kati ya wagonjwa 20 waliothibitishwa kuwa na Ebola nchini Uganda tangu mwezi Mei, wengi walikuwa wametokea DRC. Hata hivyo, mamlaka zinasema hatua za haraka zilisaidia kuzuia maambukizi makubwa ndani ya nchi.

    Wakati huo huo, DRC inaendelea kukabiliana na changamoto za usalama, uhamaji wa watu na ugumu wa kufuatilia mawasiliano ya wagonjwa, hali ambayo imechangia kuenea kwa virusi hivyo katika baadhi ya maeneo yaliyoathirika.

    Licha ya kutangaza kutokuwa na wagonjwa wa Ebola kwa sasa, Uganda imeendelea kuimarisha uchunguzi mpakani na imetuma wahudumu wa afya nchini DRC kusaidia juhudi za kukabiliana na mlipuko huo, huku ikisisitiza kuwa tishio la ugonjwa huo bado halijaisha.

    Soma Zaidi:

  2. Mwanamke alipua bomu mgahawani Urusi, watatu wafariki

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Watu watatu wamefariki dunia na wengine 21 kujeruhiwa baada ya bomu lililotengenezwa kienyeji kulipuka katika mgahawa wa Kiitaliano jijini Moscow, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya serikali ya Urusi vilivyonukuu maafisa wa usalama.

    Mlipuko huo ulitokea majira ya saa nane usiku kwa saa za Moscow katika eneo la Kudrinskaya, karibu na katikati ya jiji.

    Kamati ya Kitaifa ya Kupambana na Ugaidi ya Urusi (NAK) imesema mwanamke aliyekuwa amebeba vilipuzi alijaribu kuingia ndani ya mgahawa huo lakini akazuiwa na mlinzi wa usalama. Kifaa hicho kililipuka na kusababisha vifo vya mwanamke huyo, mlinzi pamoja na mteja mmoja wa mgahawa huo.

    Mgahawa huo, uliopo ndani ya moja ya majengo maarufu ya enzi ya Stalin jijini Moscow, ulikuwa ukiandaa hafla binafsi wakati wa tukio hilo.

    Mamlaka hazijatoa taarifa kuhusu orodha ya wageni waliohudhuria hafla hiyo wala kueleza ni nani aliyelengwa na shambulio hilo.

    Mashahidi wamesema waliona watu wakitolewa eneo la tukio wakiwa wamejaa damu kufuatia mlipuko huo.

    Ripoti za awali zilidai mlipuko ulitokea jikoni, lakini baadaye uongozi wa mgahawa ulisema kuwa "tatizo lilitokea nje ya jengo."

    Video iliyochapishwa na shirika la habari la RIA ilionyesha maafisa wa usalama wenye silaha nzito wakiwa eneo la tukio, ambalo lilikuwa limezingirwa na kuzuiwa kwa umma.

    Katika miaka ya hivi karibuni, maafisa kadhaa waandamizi wa jeshi la Urusi wameuawa ndani na maeneo ya karibu na Moscow, huku serikali ya Urusi ikiilaumu Ukraine kwa mashambulizi hayo.

    Pia unaweza kusoma:

  3. Mashambulizi yasitishwa: Trump aitaka Iran kufanya makubaliano haraka

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema amesitisha mpango wa kufanya mashambulizi dhidi ya Iran kwa sharti kwamba makubaliano yafikiwe "haraka" kati ya pande hizo mbili.

    Kupitia ujumbe wake kwenye mtandao wa Truth Social, Trump alisema aliamua "kufuta shambulio hilo, mradi tu iwezekane kufikiwa kwa MAKUBALIANO kwa haraka", ambayo yatajumuisha kufunguliwa mara moja kwa Mlango wa Bahari wa Hormuz na kumalizika kwa kile alichokiita "tishio la nyuklia la Iran."

    Trump alisema uamuzi huo ulifikiwa kwa ushirikiano na Israel. Kauli hiyo imekuja wakati vyombo vya habari vya Marekani vikiripoti kuwa Marekani ilikuwa ikifikiria kufanya mashambulizi mapya na makali dhidi ya Iran mwishoni mwa wiki.

    Awali, Iran iliishutumu Marekani kwa kuongeza mvutano katika eneo hilo, ikionya kwamba taifa lolote la kikanda litakaloshirikiana na Marekani "litamezwa na vita" hivyo.

    Katika ujumbe wake, Trump alisema Marekani iko "tayari kabisa kwa hatua za kijeshi" dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, akidai kuwa nguvu, uwezo wa kijeshi na vitisho vya Marekani vinafikia kiwango ambacho hakijashuhudiwa tangu Vita vya Pili vya Dunia.

    Hata hivyo, alisema aliamua kusitisha mashambulizi hayo baada ya kuombwa na Iran pamoja na baadhi ya mataifa ya Mashariki ya Kati kusubiri ili kutoa nafasi kwa mazungumzo ya kufikia makubaliano.

    Trump pia alidokeza kuwa hatua imepigwa katika mazungumzo hayo, akisema kuwa "misingi ya makubaliano tayari umefikiwa."

    "Hatua hii itajumuisha kufunguliwa mara moja, kikamilifu na bila masharti kwa Mlango wa Hormuz, pamoja na kumaliza tishio la nyuklia la Iran," Trump aliandika.

    Soma Zaidi:

  4. Hujambo. Karibu katika matangazo yetu ya mubashara ya tarehe 2/08/2026. Mimi ni Asha Juma.