Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Moja kwa moja, Mamia wakamatwa Ufaransa katika machafuko yaliyofutia fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya

Maelfu ya maafisa walijaribu kudhibiti ghasia huku umati wa mashabiki - baadhi wakiwasha moto mitaani- kushangilia ushindi wa PSG dhidi ya Arsenal.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Ambia Hirsi

  1. Israel yatangaza kudhibiti Kasri la Beaufort nchini Lebanon

    Jeshi la Israel leo (Jumapili) limetangaza kuwa limekuwa likipanua operesheni zake za ardhini kusini mwa Lebanon, baada ya kuvuka Mto Litani, na kuashiria kuwa limechukua udhibiti wa Kasri ya Beaufort.

    Msemaji wa jeshi Avichai Adraee aliandika kupitia jukwaa la X kwamba majeshi ya Israel yalivuka Mto Litani na kupanua mashambulizi yao dhidi ya Hezbollah kaskazini mwa mto huo, huku operesheni zikijumuisha maeneo ya ziada.

    Adraee alisema kwamba alianzisha "operesheni kubwa katika Milima ya Shaqif na eneo la Wadi Saluki siku kadhaa zilizopita," kama sehemu ya "kuimarisha udhibiti wa operesheni kusini mwa Lebanon na kuondoa tishio la moja kwa moja dhidi ya Galilee Panhandle na mji wa Metula."

    Amedokeza kuwa idadi kubwa ya wanajeshi wake wameanza mashambulizi "ili kupanua safu ya mbele ya ulinzi," na kuongeza kuwa vikosi vyake vinafanya kazi "karibu na Nabatieh, ambayo ni moja ya ngome kuu za kundi la kigaidi la Hezbollah kusini mwa Lebanon, na yuko tayari kuendelea na mashambulio akilazimika kufanya hivyo."

    Wakati huo huo jeshi la Israel limetangaza kuwa limeshambulia miundo mbinu ya Hezbollah katika mji wa Tiro na maeneo mengine kusini mwa Lebanon.

    Soma zaidi:

  2. Ebola inasambaa kwa kiwango cha 'kutisha sana' DR Congo, MSF yaonya

    Kuenea kwa kasi kwa ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kumezua hali ya "wasiwasi", shirika la matibabu la Médecins Sans Frontières (MSF) limeonya.

    Akiongea wiki mbili baada ya mlipuko huo kutangazwa na Shirika la Afya Duniani (WHO), naibu mkurugenzi wa MSF Dk Alan Gonzales alisema kamwe "kesi nyingi" hazijawahi kurekodiwa hivi karibuni.

    Kauli yake inakuja wakati mkuu wa WHO Dk Tedros Adhanom Ghebreyesus, alipotembelea mkoa wa Ituri mashariki mwa Congo - eneo lililoathiriwa zaidi - kuongoza harakati za kudhibiti virusi.

    Takribani watu 246 wamefariki kutokana na ebola huku wengine zaidi ya 1,000 wakishukiwa kuwa na virusi ugonjwa huo.

    Nchi jirani ya Uganda imeripoti kifo kimoja na kuthibitisha watu wameambukizwa.

    "Wiki mbili baada ya kutangazwa kwa ugonjwa wa Ebola katika Mkoa wa Ituri, hali inazidi kuwa mbaya," Gonzalez alisema katika taarifa siku ya Jumamosi.

    Ebola ni ugonjwa adimu lakini hatari unaosababishwa na virusi.

    Virusi vya Ebola kwa kawaida huwapata wanyama, hasa popo, lakini binadamu huambukizwa wakati pale watu wanapokula au kushika wanyama walioambukizwa.

    Huchukua siku mbili hadi 21 kwa dalili kujitokeza. Dalili huanza ghafla na kufanana na mafua, kama vile homa, maumivu ya kichwa, na uchovu.

    Maelez zaidi:

  3. Kenya yathibitisha kushirikiana na Marekani katika ujenzi wa kituo cha Ebola

    Serikali ya Kenya imethibitisha kuwa inaanzisha kituo cha karantini ya Ebola kwa ushirikiano na Marekani katika katika kambi ya kijeshi iliyopo Kaunti ya Laikipia.

    Katika taarifa iliyotolewa Jumamosi, Waziri wa Afya wa Kenya alisema kuanzishwa kwa kituo hicho kutaimarisha ufuatiliaji, kuwatenga walioambukizwa, na uwezo wa kukabiliana na hali ya dharura.

    "Uwekezaji huu utaimarisha usalama wa afya ya Kenya kwa kuboresha uwezo wa maabara, miundombinu ya afya, ufuatiliaji wa magonjwa, mifumo ya kukabiliana na dharura, na utayari wa wafanyikazi zaidi ya tishio la sasa la Ebola," wizara ilisema.

    Tangazo hilo linakuja siku kadhaa baada ya mahakama ya Kenya kuzuia kwa muda mpango ya kuanzisha kituo cha karantini cha Ebola kinachohusishwa na Marekani nchini humo, wakati ambapo kituo hicho kilitarajiwa kuanza kazi.

    Chini ya makubaliano na Kenya, Marekani ilikuwa imepanga kutumia kituo hicho chenye vitanda 50 kuwatibu Wamarekani walioathiriwa na Ebola katika eneo hilo.

    Soma zaidi:

  4. Mamia wakamatwa Ufaransa katika machafuko yaliyofutia fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya

    Zaidi ya watu 400 wamekamatwa kote nchini Ufaransa kufuatia ushindi wa Paris Saint-Germain (PSG) kwenye fainali ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Arsenal usiku wa jana huko Budapast, Hungary.

    Maelfu ya maafisa walitumwa kudhiditi machafuko yaliyotatiza huduma za mabasi, treni na reli katika mji mkuu Paris.

    Polisi walirusha vitoa machozi kutawanya umati wa watu katikati mwa jiji huku baadhi yao wakijeruhiwa katika vurumai hilo

    Video zilizonaswa jijini Paris na kusambazwa mitandaoni zinaonyesha miali ya moto ikizimwa, baiskeli zikiwaka barabarani na waltu waliokuwa wapiga kelele wakivunja vioo mbele ya duka moja.

    Eneo maarufu la Champs-Élysées lilifurika na mashabiki muda mfupi baada ya timu ya Ufaransa kuinyuka Arsenal kupitia mikwaju ya penalti. Mapema Jumamosi kulikuwa na makabiliano kati ya polisi na mashabikii waliojitokeza kutazama fainali kwenye skrini kubwa katika uwanja wa PSG wa Parc des Princes.

    Polisi wanasema magari sita, biashara kadhaa na maeneo la kuegesha mabasi yaliharibiwa wakati wa machafuko hayo..

    Vurugu sawa na hizo zilishuhudiwa wakati PSG iliposhinda kombe hilo mwaka jana, ambapo sherehe za ushindi ziligeuka kuwa machafuko.

    Waziri wa Mambo ya Ndani Laurent Nuñez amasema mwaka huu, mamlaka ilikuwa imejiandaa vilivyo kudhibiti tukio kama hili likijitokweza.

  5. Karibu wa Matangazo ya moja kwa moja.