Hezbollah na Israel zalaumiana kwa kuvunja makubaliano ya kusitisha mapigano
Jeshi la Israel na kundi la Hezbollah wameshutumiana kwa kuvunja makubaliano ya kusitisha mapigano.
Awali, Israel ilisema ilifanikiwa kuzuia makombora kadhaa yaliyofyatuliwa kutoka Lebanon, huku ving’ora vya tahadhari vikisikika katika eneo la Shtula.
Kwa upande wake, Hezbollah ilithibitisha kupitia Telegram kwamba ililenga eneo hilo kwa shambulio la makombora.
Katika taarifa yake kupitia mtandao wa X, IDF ilisema pia imewaua watu watatu inaowataja kama “wanamgambo wa Hezbollah” baada ya kushindwa kufyatua kombora kuelekea ndege ya Jeshi la Israel.
IDF pia ilidai kuwa katika matukio mawili tofauti, Hezbollah ilifyatua makombora dhidi ya wanajeshi wake walioko kusini mwa Lebanon, ikisema kuwa hatua hizo ni “uvunjaji wa wazi wa makubaliano ya kusitisha mapigano.”
Hata hivyo, Hezbollah ilijibu Alhamisi jioni ikisema ilifyatua makombora kuelekea kaskazini mwa Israel kama kujibu kile ilichokiita “uvunjaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano” uliofanywa na Israel.
Wakati huohuo, Shirika la Habari la Taifa la Lebanon linaripoti kuwa Israel imefanya mashambulizi katika mji wa Tyre ulioko kusini mwa nchi hiyo asubuhi ya leo.
Unaweza kusoma pia: