Trump: Utawala wenye nguvu umeondolewa, sasa unaongozwa na kiongozi wa jinsia moja
Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa wakati wa uongozi wake, "utawala ambao zamani ulikuwa wa kutisha, wenye nguvu na uliokuwa ukiishambulia Marekani bila kukoma uliondolewa madarakani," ingawa hakuitaja Iran moja kwa moja.
Akizungumza katika hafla ya Chama cha Waandishi wa Habari wa Ikulu ya White House, Trump alisema viongozi wa zamani wa utawala huo waliondolewa na sasa nchi hiyo inaongozwa na "dikteta ambaye anashiriki mahusiano ya jinsia moja anayekabiliwa na migogoro ya ndani."
Kauli za Trump zinaonekana kuirejelea Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Mojtaba Khamenei.
Hata hivyo, hakutoa ushahidi wa kuunga mkono madai hayo, na hapo awali pia amewahi kutoa madai yanayofanana kuhusu kiongozi wa Iran.
Unaweza kusoma;