Ashtakiwa kwa mauaji na unyanyasaji wa kingono dhidi ya mtoto wa miaka mitano
Mwanaume mmoja ameshtakiwa kwa mauaji na makosa mawili ya unyanyasaji wa kingono kufuatia kifo cha msichana wa miaka mitano nchini Australia.
Mwili wa msichana huyo, anayejulikana kama Kumanjayi Little Baby, jina la bandia alilopewa na familia yake kwa sababu za kitamaduni baada ya kifo chake ulipatikana Alhamisi baada ya siku kadhaa za msako mkubwa wa polisi.
Jefferson Lewis, mwenye umri wa miaka 47, alishtakiwa kwa mauaji yake Jumamosi usiku na anatarajiwa kufikishwa mahakamani Jumanne katika mji wa Darwin.
Watu watano wamekamatwa kufuatia ghasia za vurugu zilizotokea Alice Springs baada ya kifo cha mtoto huyo.
Kamishna wa Polisi wa Northern Territory, Martin Dole, alitangaza mashtaka dhidi ya Lewis Jumapili asubuhi.
“Bado hili ni tukio linaloumiza sana, na mawazo yetu yako pamoja na familia ya Kumanjayi, wapendwa wake na jamii pana iliyoathiriwa kwa kiasi kikubwa na matukio haya,” alisema.
Dole aliomba jamii iheshimu mchakato wa kisheria.
Inaripotiwa kuwa Jefferson Lewis alishambuliwa katika mji wa Alice Springs kabla ya kukamatwa Alhamisi.
Unaweza kusoma;